Friday, October 24, 2014

AMANI NA IWE KWENU

Nawasalimu katika jina la YESU,AMANI na iwe kwenu.Ni furaha yangu na imani yangu kuwa mnaendelea vizuri katika KRISTO YESU.Ni mwaka mwingine wa masomo na hongera kwa wale walioingia mwaka wa 3 na wa  2 na wale wageni wa mwaka wa kwanza.Ni wakati mwingine wa kutafakari kitu gani tumemfanyia MUNGU  na kitu gani tunapaswa kukifanya kwa nafasi hii aliyotupa.
   Leo hii napenda tukumbushane juu ya huduma za ujumla (collective) na huduma binafsi (Individual).Huduma izo zote zinahitajika kufanyika kwa nguvu zote,mfano kutoa fungu la kumi ni agizo binafsi ambalo linakupasa ulifanye,kushirik huduma za kanisa ni huduma za pamoja na wakati mwingine inaweza kuwa binafsi.Jipange utumike kwa nguvu zako,muda wako,akili zako,mawazo yako.Ndipo Musa akasema tutakwenda na mali zetu  na kila kitu chetu..

0716047700

No comments:

Post a Comment