Saturday, May 17, 2014

UCHUMBA NA NDOA... MWASHAMBWA



                                
 
 Lizick mwashambwa ..(aliye kushoto)
  NDOA NA UCHUMBA
Math 7:21- yeye afanyaye mapenzi ya baba yangu ndiye atakaye okoka.
Luka 6:46(kufanya maagizo ya Mungu)
Moja ya mapenzi ya Mungu ni kuona watu wanaoa na kuolewa, hivyo kuhitaji kuoa au kuolewa si dhambi madam zingatia (Mhu 3:1). Hata hivyo biblia haijaweka wazi kwamba ni kwa wakati gani au umri gani inatakiwa mtu aoe au kuolewa ila cha msingi ni kutambua kwamba Mungu ni wa utaratibu(1Thes 3:6-7). Hata hivyo, haitoshi neon la Mungu linasema ‘’KUMCHA BWANA NI CHANZO CHA MAARIFA’’(Mith 1:7), nini maana ya neon ‘maarifa’, zipo maana nyingi za neon maarifa, miongoni mwazo ni; akili ya ugunduzi, hivyo wewe mwenyewe kama mtu uliye okoka na mwenye maarifa unapaswa kugundua wakati wako wa kuoa au kuolewa kwa kuwa ni miongoni mwa kutimiza mapenzi ya Mungu, hivyo kutohitaji kuoa au kuolewa wakati una sifa za kufanya hivyo ni kudharau mapenzi ya Mungu wazi wazi na kibaya zaidi unajikuta unaangukia katika uasi wa macho na mawazo(Math 5:28). ZINGATIA: hata hivyo watumishi wa Mungu husema kuhitaji kuoa au kuolewa ni WITO. Hata mimi kwa ufahamu wangu nakubali hiyo dhana kwani unakuta mtu ni Yule Yule siku zingine zote alikuwa hahitaji suala hilli mbali na hapo alikuwa hataki kuzungumzia na  kusikia habari yoyote kuhusu jambo hili. Lakini wio wake ukifika utamuona yeye mwenyewe anaanza kuhitaji ,kuzungumzia na hata kupenda kusikia habari hizi, hivyo kwa mtu huyo ajue tayari kwa wakati umefika akiachana na vipindi vya mpito vya ukuaji wa mwili kwa maana ya balehe na kupevuka kwa kuwa hiki ni kipindi hatari sana ambacho kijana mara nyingi huendeshwa na mawazo ya kawaida na hisia za mwili kabisa(Gal 5:19).
LAKINI, nasikitika kwa vijana wenzangu ambao wamejitunza katika maisha ya kiroho na kimwili tangu walipookolewa, lakini wakifikia kipindi hiki cha kupata wito wa kuoa au kuolewa huwa wanajiuliza yafuatayo;
a)      Tumevamiwa na shetani
b)      Tumeanza kurudi nyuma
c)      Tunaelekea kutenda dhambi
d)     Tumeanza kupenda dunia
Hata hivyo wengi wetu huanza kuikataa hali hiyo na kuikemea kwa gharama kubwa hata kwa kufunga na kuomba. Lakini kwa kuwa neon la Mungu linasema ‘’kwa kuwa umekataa maarifa name nimekukataa wewe’’(Hosea 4:6-8), nasikitika kusema kwamba, kwa kuwa hapa yunapingana na mpango wa Mungu, mwisho wa vijana wengi waliookoka na si kuokoka tu na hata walioonja neema ya kuitwa watumishi wa Mungu huwa wanarudi nyuma kwa kasi kubwa na kuacha jamii, kanisa, wazazi na marafiki wetu wameshika tama zao na vidonda visivyo ponyeka mioyoni mwao na kukamilisha msemo usemwao na wengi wanaodhihaki wokovu kwamba huwezi kuokoka ukiwa kijana au kuokoka ni hatua ya kupitia katika maisha ya mwanadamu kama ilivyo kutambaa kwa motto mdogo n.k
Lakini kukataa wito huu wakati unajua ni agizo la Mungu(Mwa 1:29) ni sawa unahisi njaa baadala ya kuomba msaada wa chakula unaanza kukemea sijui kama unaweza kufanikiwa.
Samahani kwa wachungaji na watumishi wa Mungu wengine kwa kuwa nami ni kijana sikupaswa kuandaa somo hili, lakini kulingana na jambo hili linavyo athiri vijana wenzangu kwa kasi ni kubwa mpaka sasa kuna vijana wenzangu wengi waliorudi nyuma, lakini zaidi wako vijana watatu wameshapotea kabisa katika huduma.ila ungepata neema ya kuyajua maisha yao kabla ya kurudi nyuma ungelia machozi na siwezi kuwasahau kwa jinsi ambavyo tulishirikiana nao katika kumtumikia Mungu. Ni kwa sababu ya usalama tu majina yao yamehifadhiwa ningewataja dhahiri. Hivyo, nimepata msukumo wa kuaandaa somo hili sijui kama ni mawazo yangu au ni maelezo ya Mungu. lakini katika yote mungu anihurumie na kuniongezea neema.
Ndugu zangu vijana mliookolewa ikumbukwe kwamba pamoja na kuokoka mwili huwa  unabaki na utaratibu wake wa kawaida. Kinacho takiwa ni kuushinda, katika somo la baiolojia tunasema kinacho takiwa ni kuufanya mwili kuwa recessive  na roho kuwa dominant, hata hivyo kuna baadhi ya kanuni za mwili huwa zinabaki pale pale kama kuhitaji kula, kuoga , kunywa, kulala, kuvaa n.k. cha msingi kupitia (Mith 1:7) unapaswa kujiuliza yafuatayo kulingana na mifano tajwa hapo juu
       I.            Unatakiwa kula nini na kwa mda gani?
    II.            Unatakiwa kuoga nini na wapi?
 III.            Unatakiwa kunywa nini na eneo gani?
 IV.            Unatakiwa kulala wapi na mda gani?
    V.            Unatakiwa kuvaa nini, wapi na kwa mda gani(Math 6:15-19)
Kadhalika mwili huwa unafika mahali unahitajikukamilishwa kwa kuoa au kuolewa(Mwa 2:21-24). Cha msingi hapa ni kwamba kuhitaji kupata mwenzi wa maisha si dhambi ila nani wa kuwa mwenzi wako, yuko wapi, utampataje na ni lini? Katika maswali hayo na mengine mengi ambayo vijana huwa tunajiuliza katika eneo hili basi karibu tufuatane hapa chini na tuone namna ya kupata majibu.
A.    IMANI NA SUBIRA KATIKA KUOA NA KUOLEWA
Baada ya kuona kwamba  kuhitaji kuoa au kuolewa siyo dhambi bali ni hatua ya kupata mwenzi wako katika maisha(1Kor 11:11). Cha msingi unapaswa kuwa na subira pamoja na imani(Ebr 11:1-6) ZINGATIA , vyovyote vile tulivyo lazima tuamini kwamba kila kaka ana mke wake na kila dada ana mme wake mmoja katika Bwana na yupo mahali flani hata kama bado hatuja wafahamu katika macho ya kawaida na bila kujali falsafa ya takwimu za dunia kwamba wanawake ni wengi kuliko wanaume. HAPA MWAMINI MUNGU KUWA YUPO MWENZI WAKO HATA KAMA HUJUI ALIKO AU NI NANI
a)      Bila kujali gharama za maisha au uchumi wako
b)      Bila kujali sura, umbile, rangi, kimo, kabila, asili, elimu,au ulemavu wako yupo wa kufanana na wewe(Mwa 2:18) NB: mimi binafsi najua Mungu humtoa mtu chini na kumpeleka juu, wengine wanakataa kuolewa au kuoa kwa kuangalia vigezo vya uchumi, gari, elimu nk. Lakini shuhuda za wengi waliofanya jambo hili katika njia za Bwana wanasema maisha mazuri ya ndoa ni yale watu wanaanza chini na kwenda juu.
B.     IMANI YA MUNGU NI LAZIMA IAMBATANE NA SUBIRA    pamoja na uzuri wa jambo hili la kuoa au kuolewa katika Bwana ni lazima kabla ya tendo hilo mhusika awe binti au kijana asubiri kwanza wakati Mungu anafanya mpango kwa ajili yake(Yak 5:11)  HAPA NDIPO VIJANA WENGI TUNAPO KOSEA, njia pekee ya kupata mwenzi wako wa maisha ni KUOMBA KWA IMANI TU, hata hivyo kwa binti akiomba hata akipata msukumo juu ya kijana flani haruhusiwi kwenda kumwambia ila asubiri, kwa upande wa kijana wa kiume zipo hatua tatu za kufuata (1)kuomba (2)kutafuta kwa maelezo ya Roho mtakatifu (3) kutoa taarifa kwa binti, baada ya kutoa taarifa kwa binti, binti mwenye busara na makini hata kama anajua ndiye aliye pata msukumo kwake ataomba mda wa kwenda kumuuliza Mungu kwa usahihi zaidi, ila siyo kuleta usumbufu usiokuwa na maana na wewe kaka ukisha ambiwa subiri siyo kukasirika na kuchukua maamuzi ya haraka. Binti baada ya kumuomba Mungu kwa usahihi na kujua kwamba jambo hilo ni kweli unapaswa kutoa taarifa kwa UTARATIBU. Ni vizuri taarifa zipitie kwa watumishi wa Mungu kwanza ili wawape utaratibu namna ya kwenda na jambo hili kabla ya ndoa maana  uzoefu unaonyesha kwamba baada ya hawa wawili kuridhiana huwa kunakuwa na raha ya ajabu ambayo inaweza kuwapelekea katika kumkosa Mungu wakikosa usimamizi wa karibu wa watumishi wa Mungu wakati wa uchumba wao(Math 7:7).
USHAURI-kwa kuwa jambo hili utafiti wa kisasa unaonyesha kwamba watu  wengi wakiwemo wenye uchumi wa juu na walio na elimu ya juu walishashindwa kabisa na kujikuta wanalia kilio kisicho na msaada “MAJUTO NI MJUKUU” hivyo mshirikishe baba yako wa kiroho pamoja na watumishi wa kweli wa Mungu wachache ili usije ukakwea penginepo(1Sam 3:1-11).
Samahani sitazungumzia kwa undani juu ya ndoa ila niombee siku nikipata neema nitazungumzia hilo, lakini kwa kifupi kwa kuwa uchumba unatupelekea kwenye ndoa ni muhimu ujue misingi mikuu mitano ya ndoa ya mtu aliyeokoka.
       I.            Wote wawili wawe hawajawahi kuingia katika ndoa, au mmoja wapo au wote wamefiwa na wenzi wao na si VINGINENYO.(1kor 7:8-9,38-39)
    II.            Ruhusa ya binti (Mwa 24:57-58)
 III.            Ruhusa ya wazazi wa binti- inaweza kuambatana na kutoa mahali maadam uruhusiwe na wazazi wa binti, hata usipo toa mahali lakini ukiruhusiwa na wazazi wake haina shida, hakuna kipimop maalum cha mahali itategemeana na utakavyo jieleza (1Kor 7:36)
 IV.            Baraka za wazazi wa rohoni(Mwa 1:27-28, Hes 6:24-27)- huu msingi wa nne ni kwa watu waliookoka na ni muhimu sana kuliko unavyo dhani. Baada ya watu kufunga ndoa wakiwa kanisani au mahali pengine ni MWIKO kusema nilikosea kwa hiyo nafunga ndoa tena huo ni UZINIFU zaidi ya ule unaofanywa na mataifa,
    V.            Kuambatana katika maisha kwa maana ya kuwa mwili mmoja(Mwa 2:24) TAHADHARI- MWIKO MWEBRANIA KUWA KATIKA MAHUSIANO YA KIMAPENZI(UCHUMBA) NA MMISRI, MWISRAELI NA MYEBUSI(2Kor 6:14-18); katika tahadhari hii ukumbuke kilicho mtokea SAMSONI kwa DELILA na kilicho mtokea SULEMAN kwa wanawake wa kigeni(wasiookoka)(1Fal 11:1-4, Amu 16:1-31)
Nimalizie kwa kukutia moyo binti au kaka kama utapata mwenzi wako ambaye ni mcha Mungu yaani anaye mhofu Mungu kuna faida kubwa sana za kiroho na kimwili neon la Mungu linasema hayo na watu wachache wal;iofanikiwa katika hili suala, hizi ni baadhi ya faida hizo
a)      Nguvu za kiroho huongezeka pale tunapokuwa wawili yaani mme na mke katika Bwana kwa kupitia faraja, ushauri na ushirikiano na kinyume chake linaweza kuwa jibu(Kumb 32:30, Yosh 23:10, Mhu 4:9-12)
b)      Utapata nguvu zaidi ya kushinda dhambi inayotesa ulimwengu kipekee, zinaa au uasherati(1Kor 7:1-7).
MWISHO- UBARIKIWE KIJANA MWENZANGU, Mungu akinipa neema tutaonana kwa miaka ijayo katika somo liitwalo “MALIPIZO YA NDOA”
       Ni mimi   Mtumwa wa Yesu………….
                       Mwashambwa  N  Liziki
Kwa maswali, maoni na msaada wa maombi tumia
     0752 267 292,  P.O.BOX 85 MBEYA,  lizikineckson@gmail.com



No comments:

Post a Comment