Thursday, December 13, 2012

UMUHIMU WA KUWA NA AGANO NA MUNGU




SEHEMU YA PILI (2).
Wiki iliyopita tuliachia katika maana ya Agano,Wiki hii tunaendelea kuona jinsi maagano ya kibinadamu yanavyowekwa pamoja na maagano ya ki MUNGU yanavyowekwa.
A: MAAGANO YA KIBINADAMU
Maagano ya kibinadamu ni makubaliano yanayofikiwa baina ya watu kila upande upande ukiwajibika kutimiza makubaliano yaliyopo katika  Agano lao.
 Maagano yanawekwa katika mazingira gani?
Maagano yanawekwa katika  hali ya utulivu pasipo kulazimishwa.Lugha ya kisheria inaonyesha mkataba uwekwe pasipo (Fraud,Misrepresentation,Undue influence.)
Kitu gani kinalinda Agano (Makubaliano)?
Makubaliano yanalindwa na aidha katika karatasi (document) maalumu ambayo kila upande unabaki na nakala (copy) moja..Mahakama itaangalia nakala za makubaliano yale,ili kumtia hatiani Yule aliyeshindwa kutimiza yale yaliyo katika makubaliano.
B:MAAGANO YA KIMUNGU
Ni patano kati ya mtu na MUNGU.Kwa watu wengi haieleweki,wengi wanajiuliza ni jinsi gani MUNGU anaweza kuweka agano na mwanadamu.Ila ni ukweli kuwa walioweka maagano na MUNGU walipata faida kuu,angalia ( Nehemia 1:2-11,7:1-3)
Maagano yanawekwa katika mazingira gani?
Maagano ya ki MUNGU yanawekwa katika MAOMBI,maana ndipo tunapoweza kusema na MUNGU wetu.Kama ilivyo katika makubaliano ya kibinadamu hata katika maombi pia utulivu unahitajika maana yale mtakayokubaliana ndiyo yatakayopaswa kufuatwa.(Mwanzo 24:43-48).
Kitu gani kinalinda Agano (Makubaliano)
Maagano ya ki MUNGU yanalindwa na kutunza yale uliyomuomba MUNGU.Tazama Isaya 43:26 “unikumbushe” ina maana utunze agano “maombi”.
Itaendelea……….



1 comment: