Saturday, May 17, 2014

SOMO LA MAHUSIANO- kutoka kwa mzawa wa injili



                          mzawa wa injili

MAHUSIANO
Mzawa wa injili,, ninawakaribisha katika kulianza somo letu zuri la mahusiano. Kwa undani zaidi kuhusu somo hili na mengine mengi kuhusu mzawa wa injili tembelea  live bila chenga gospel blogspot.com  au mzawa wa injili gospel forever blogspot.com.

    UTANGULIZI
Mahusiano ni muhimu na lazima katika maisha. Hatuwezi kuishi pasipo mahusiano. Hata hivyo, mahusiano yaweza kuwa dhana ya kutuumiza au kutupa amani na  hii hutegemeana na aina ya mahusiano husika. Katika somo hili Mungu amenipa Neema kuzungumzia kwa undani  mahusiano juu ya vijana ambao hawajaoa ama kuolewa… unajua ni kwa nini (1Yoh 2:14),, vijana wanazo nguvu na hivyo Mungu anahitaji awatumie, lakini shetani anahitaji awatumie pia. Na pia biblia inatuonya kumkumbuka Mungu siku za ujana wetu (Mhu 12:1).
        
Mahusiano mabaya na mazuri
Ni swali ambalo liko katika vichwa vya watu wengi,, yapi ni mahusiano mazuri au mabaya kwa kijana. Ndugu zangu, katika mtazamo wa Biblia nitaeleza kidogo na ROHO akupe neema ya kuelewa. Vijana wengi waliookoka wamejikuta wakianguka katika dhambi kwa kushindwa kuchagua kwa usahihi ni aina gani ya mahusiano wawe nayo. Vifuatavyo ni baadhi ya vigezo unavyoweza kutumia kujua kama mahusiano uliyo nayo ni sahihi au siyo.

Yanampendeza Mungu?
Kila jambo linalo fanyika nje ya upendo wa Mungu ni dhahiri kuwa litampelekea mhusika katika majuto na aibu. Unaweza kulipima hili kupitia usemi na mwenendo wenu kwa ujumla katika mahusiano yenu. Biblia inasema mazungumzo mabaya huharibu tabia njema(1Kor 15:33). Mazungumzo mabaya,na dalili yoyote ya dhambi itakupelekea kumkosea Mungu na kujutia maamuzi yako. Kwa hiyo, mahusiano yoyote ambayo yako nje ya kusudi la Mungu hayafai na yanapswa kuepukwa. Tumia muda mwingi katika kuomba na Mungu lazima akuonyeshe cha kufanya.

Una amani ya kristo?
(Kol 3:15)..Ni lazima pia upime kama amani ya kristo ina ruhusu wewe kuwa katika mahusiano hayo. Hapa pia naomba nieleweke kuwa si kila amani iliyo ndani yako yatoka kwa kristo. Kuna watu wanaotumia mwanya huu kujihalalishia mahusiano yasiyo halali kwa kudai kuwa amani ya kristo ina waruhusu kumbe ni matakwa yao na mwisho wao huwa ni kujuta tu. Naomba nikupe ushuhuda huu “ nikiwa kidato ch nne, binti mmoja alinifuata na kuniomba ushauri juu ya kijana mmoja aliye kuwa anamfuata akitaka kumuoa ila alikuwa hajaokoka. Binti Yule nilipomuuliza anajisikiaje alisema ana amani kabisa lakini niligundua haikuwa amani ya kristokwani amani ya kristo huwa haina utata kwa ndani.. nilimpa ushauri wa kibiblia na kumpa wiki moja ya maombi alipime jambo hilo mbele za Mungu. Nashukuru Mungu alimpa neema na kumjulisha kuwa mahusiano aliyokuwa nayo si sahihi akaamua kuyavunja na baadaye amani ya kristo ilijaa ndani yake. Mwaka jana mwezi wa pili alifunga ndoa takatifu…” biblia inatofautisha amani ya kristo na ya dunia(Yoh 14:1…) hakuna mahusiano ya mapenzi kati ya aliyeokoka na ambaye hajaokoka (2Kor 6:15-17).

Umemhakikisha Mungu?
Hata kama mahusiano yenu ni ya waliookoka wote ni lazima pia umhakikishe Mungu uone kuwa yeye ndiye ameruhusu hayo mahusiano au la. Mpendwa jitahidi kumhakikisha mungu katika maisha yako. Ni vyema kutambua kuwa si kila aliyeokoka anaweza kuwa mke/ mme wako. Biblia inasema kuwa Mungu akatwaa ubavu mmoja kutoka kwa Adam akamtengeneza Hawa mke wake (Mwa 1:26-27). Hivyo, kuna mtu special wa kwako  ambaye Mungu amemwandaa kwa ajili yako. Mhakikishe Mungu kwa maombi na ishara, yaweza kuwa isiwe mara moja(angalia alicho kifanya Gideoni( Amu 6:36)). Ukisha gundua kuwa siyo Mungu mwombe Mungu akupe hekima ya kuyakomesha mahusiano hayo katika njia ambayo haitaleta madhara yoyote kwako na kwa mwenzako.
NB: Ni hatari kubwa kuendelea katika mahusiano ambayo unajua kabisa Mungu hajayaruhusu, eti, kwa sababu unafikiria itakuwaje ukiyavunja, au mwenzako atakuelewaje? Kumbuka ndugu yangu haya ni maisha yako hivyo usiyachezee baadaye ukaja kujuta, kwani Mungu kama hajakubali hautakuwa na haki ya kumdai chochote baadae mambo yakiharibika kwani ulijua unacho kifanya. Usifanye huruma isiyo sahihi leo ikakugharim maisha yako yote. Ukumbuke pia kuwa hata makanisan kuna ma agent wa adui wanaoletwa kwa lengo tu la kuwaangusha watumishi waliosimama katika Mungu hasa kupitia MAHUSIANO. Hivyo ni vyema uwe makini katika kila hatua unayopitia.
Pia, kuvunja mahusiano kuna gharama yake. Hii nitaizungumzia zaidi katika sehemu inayo fuata ya somo hili inayosema ‘utafanya nini mahusiano yakivunjika?
  Je ni hitaji lako kwa wakati huo?
Ni lazima ujue kwa kuchunguza kwa umakini kuwa ni hitaji lako kwa wakati huu kuwa na mke/mme. Je, uko tayari kutoka moyoni na si kwa ushawishi wa watu? Je, si kwa sababu umewaona rafiki zako wanaoa na kuolewa na wewe ukatamani? Ni muhim pia kujua kuwa hilo lililo katika wakati wako lazima liendane na wakati wa Mungu (Yoh 11:1…..) usifanye jambo wakati usio wake kwani kila jambo lina wakati wake( Mhu 3:1…)
K      u           m                 b                           u                     k                        a…….

Hakuna haja ya kulazimisha kupendwa kwani kama limepata kibali mbele za Mungu kupendwa kutakuja automatically tu. Kumbuka pia hapa nazungumzia upendo na si tama kama wengi wanavyo yachanganya mambo haya mawili.
Ndugu zangu, kwa leo naomba niishie hapa, kesho ntakuletea mwendelezo wa somo hili katika vitu hivi ‘utafanya nini mahusiano yakivunjika?’ na ‘jinsi ya kuutambua upendo wa kweli’
Mungu wangu ninaye mtumikia na Awabariki sanaa…
   MZAWA WA INJILI
Kwa maombi na ushauri tumia,
sekomu casfeta tayomi blogspot.com
0759210407

No comments:

Post a Comment