Saturday, May 24, 2014

SURA YA MUNGU-SEHEMU YA 1

kila mtu na sura yake


.................Zamani nilikuwa  najiuliza maswali mengi,najua hata wewe ulijiuliza au yamkini unajiuliza maswali hayo kila siku kuwa MUNGU kafanana vipi na mwanadamu ikiwa Biblia inasema kuwa “………na tumfanye mtu kwa mfano wetu na sura yetu ….” (Mwanzo 1:26).Hajaishia hapo tu katika injili ya Yohana 1:12 Biblia inazidi kumuweka karibu mwanadamu na MUNGU kwani inaonyesha jinsi mtu akimkubali MUNGU anafanyika kuwa mwana wa MUNGU….Kama hali ni hiyo sura ya MUNGU kama baba itafanana na mchina, mzungu, mwafrika au mhindi? Yule mheshimiwa aliyeigiza video ya maisha ya YESU amechukua umaarufu mkubwa duniani na hata watu wengine wameamini kuwa YESU yupo vile, kama hali ipo ivo kuna umuhimu wa kuijua sura ya MUNGU. Katika somo hili tutaenda kuangalia sura ya MUNGU katika mtazamo wa kibiblia zaidi,kwa nini ameonyesha umuhimu wa sisi kuwa na sura yake.Kuna mtu napendaga kumwambia “as mother as daughter, as father as son” na hili linathibitishwa na maneno haya katika Injili ya Yohana 5:19 ampapo biblia inaonyesha kuwa mwana hawezi kutenda jambo lolote mwenyewe isipokuwa amemwona baba akitenda.Hapo imeonyesha uhusiano wa mwana (YESU) na baba (MUNGU BABA)……
UTAKATIFU
Biblia inaeleza wazi katika 1Petro:15-16       “iweni watakatifu kama mimi nlivyo mtakatifu” inamaanisha nini hapo? Ni ishara kuwa MUNGU wetu ni mtakatifu na hata sura yake imejaa utakatifu.Mtazame Manoa baba wa Samsoni katika kitabu cha Waamuzi 13:22,alivostuka na kupatwa na mshangao alipomuona tu malaika wa BWANA sura yake tu ilimuweka mbali nay eye hata akajiona kuwa atakufa.Mtazame Musa katika Kutoka 33:11 jinsi biblia inavyonesha ukaribu wetu na MUNGU unajengwa kwa kuwa na sura ya MUNGU hivyo ilimuwezesha Musa kuongea na MUNGU kama mtu na rafiki yake.Ukikosa utakatifu basi umepoteza sura ya MUNGU ndio maana Adam na Eva walipomuasi MUNGU walijiona wapo uchi wamekosa sura ile ya MUNGU hata wakaanza kujitafutia mavazi ya kuvaa (mwanzo 3:7)……
Itaendelea!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Kaizer Xavier Msosa-0716047700,0759302486

No comments:

Post a Comment